پایگاه اطلاع رسانی آیت الله ابراهیم امینی قدس سره

Vazi La Hijabu La Kiislamu

Vazi La Hijabu La Kiislamu

Wanaume na wanawake, licha ya kwamba wanavyo vipengele vingi vinavyofanana, pia wanazo tabia za pekee. Mojawapo ya tabia hizi ni kwamba wanawake ni viumbe wa kuvutia, wazuri, na wanaopendwa. Ni wachangamfu, wanavutia na wanapendwa; ambapo wanaume huchangamshwa, huvutiwa na huwapenda wanawake kwa sifa zao.

Mwanaume anapomuoa mwanamke, hutamani uzuri wote na mapenzi yote ya mke wake visitiriwe kwa ajili yake tu.

Hutumaini kuwa ni yeye peke yake ndiye anayefaidi uchangamfu, mapenzi, kujishaua, uzuri, ukunjufu na kadhalika na kuwaepuka wanaume wengine kabisa. Mwanaume kimaumbile yu moto moto sana na hamvumilii mwanaume mwingine kumtazama mke wake au kuanzisha aina fulani ya uhusiano naye. Mwanaume ataona uhusiano wa karibu na mke wake na wanaume wengine kuwa ni kukiukwa kwa haki yake ya kisheria. Mume anatarajia mkewe kufuata kanuni ya vazi la kiislamu la Hijab na kwa kuwa mwepesi wa kubadilika kufuatana na tabia na maadili ya Kiislamu atashiriki katika kutunza haki yake ya kisheria.

Mwanaume yeyote aliye mwaminifu na hamasa lazima atakuwa na hamu hiyo. Tabia ya kijamii ya mwanamke ambayo imeegemezwa kwenye maadili ya Kiislamu, itaweka akili ya mume katika hali ya utulivu; kwa hiyo atafanya kazi kwa shauku kubwa ili aweze kutunza familia yake, na mapenzi kwa mke wake yataongezeka. Mwanaume wa namna hii hatavutiwa na wanawake wengine. Kinyume chake mwanaume ambaye mkewe havai Hijab ambayo ni vazi linalovaliwa na mwanamke Mwislamu na badala yake huonesha uzuri wake kwa wanaume wengine au anachanganyika nao, atatibuliwa sana. Atamuona mke wake kuwa anahusika na kukandamiza haki zake. Mume wa aina hiyo kila mara atapitia kwenye mateso na taabu na mapenzi kwa mkewe yatapungua pole pole.

Kwa hiyo, ni kwa manufaa ya jamii, na wanawake kwamba wanatakiwa kuvaa inavyostahiki na kuwa na tabia ya unyenyekevu, wanatakiwa kuonekana hadharani bila urembo na kuacha kuonesha uzuri wao kwa wengine.

Kuvaa Hijab ni wajibu wa Kiislamu. Mwenyezi Mungu Mweza wa yote anasema kwenye Qur’ani Tukufu:

    وَقُلْ لِلْمُؤْمِنَاتِ یَغْضُضْنَ مِنْ أَبْصَارِهِنَّ وَیَحْفَظْنَ فُرُوجَهُنَّ وَلَا یُبْدِینَ زِینَتَهُنَّ إِلَّا مَا ظَهَرَ مِنْهَا ۖ وَلْیَضْرِبْنَ بِخُمُرِهِنَّ عَلَىٰ جُیُوبِهِنَّ ۖ وَلَا یُبْدِینَ زِینَتَهُنَّ إِلَّا لِبُعُولَتِهِنَّ أَوْ آبَائِهِنَّ أَوْ آبَاءِ بُعُولَتِهِنَّ أَوْ أَبْنَائِهِنَّ أَوْ أَبْنَاءِ بُعُولَتِهِنَّ أَوْ إِخْوَانِهِنَّ أَوْ بَنِی إِخْوَانِهِنَّ أَوْ بَنِی أَخَوَاتِهِنَّ أَوْ نِسَائِهِنَّ أَوْ مَا مَلَکَتْ أَیْمَانُهُنَّ أَوِ التَّابِعِینَ غَیْرِ أُولِی الْإِرْبَةِ مِنَ الرِّجَالِ أَوِ الطِّفْلِ الَّذِینَ لَمْ یَظْهَرُوا عَلَىٰ عَوْرَاتِ النِّسَاءِ ۖ وَلَا یَضْرِبْنَ بِأَرْجُلِهِنَّ لِیُعْلَمَ مَا یُخْفِینَ مِنْ زِینَتِهِنَّ ۚ وَتُوبُوا إِلَى اللَّهِ جَمِیعًا أَیُّهَ الْمُؤْمِنُونَ لَعَلَّکُمْ تُفْلِحُونَ

“Na waambie Waumini wanawake wainamishe macho Yao, Na wazilinde tupu zao, na wala wasioneshe uzuri wao isipokuwa unaodhihirika. Na waangushe shungi zao juu ya vifua vyao, wala wasioneshe uzuri wao ila kwa waume zao, au baba zao au baba wa waume zao, au watoto wao, au watoto wa waume zao, au kaka zao, au watoto wa kaka zao, au wana wa dada zao, au wanawake wenzao, au iliyowamiki mikono yao ya kuume, au wafuasi wanamume wasio na matamanio, au watoto ambao hawajajua mambo yanayohusu uke. Wala wasipige chini miguu yao ili yajulikana mapambo waoliyoyafisha. Na tubuni vyote kwa Mwenyezi Mungu, enyi Waumini, ili mpate kufanikiwa. (Quran 24:31)

Kuchunga vazi la Kiislamu la Hijab na kuizingatiwa matumizi yake katika jamii kuna manufaa kwa wanawake katika vipengele vingi: Kwa kutumia vazi la Hijab, wanawake wanaweza kulinda uzuri wao wa kijamii na maadili ya ndani kwa ubora zaidi, na kujilinda dhidi ya kuwa tu kitu kilichopo kwenye maonesho.

Wanaweza kuthibitisha imani na mapenzi yao kwa waume zao, kwa ukamilifu zaidi na kwa hiyo kusaidia kutengeneza na kutunza familia yenye uchangamfu na kuzuia hisia mbaya na ugomvi wa kifamilia. Kwa ufupi, wanaweza kuvutia nyoyo za waume zao na kujiimarisha kwenye familia zao.

Kwa kuzingatia matumizi ya Hijab ya Kiislamu mitazamo isiyo ya kisheria yenye dokezo ya kutamani kutoka kwa watu wenye udhaifu huo, itakoma na kusaidia kupunguza idadi ya ugomvi, kuimarisha mizizi ya familia, na matokeo yake kutengeneza mazingira ya utulivu ndani ya familia.

Hijab ya Kiislamu ya wanawake pia itasaidia vijana wa kiume ambao hawajaoa, kutokana na kujiingiza kwenye vitendo viovu. Hivyo, kuwaepusha vijana dhidi ya mazingira yanayoamsha hisia za kutamaani mwanamke aliyevaa nguo isiyo sitiri umbo lake hali ambayo pia itawanufaisha wanawake katika jamii.

Kama wanawake wote wangefuata utaratibu wa Hijab ya Kiislamu basi, wanawake wote wangekuwa na uhakika kwamba waume zao wanapokuwa nje ya familia zao, hawangekutana na mwanamke asherati ambaye angewavutia na kumtoa nje ya familia yake.

Uislamu unatambua lengo mahususi ambalo limesababisha kuumbwa kwa mwanamke na humuona yeye kama msingi muhimu wa jamii na kupewa wajibu kwa jamii. Jamii humtaka mwanamke ajitolee katika kutekeleza wajibu wake wa kuvaa Hijab ya Kiislamu, ambayo ingeepusha uovu na upotofu wa jamii na kutengeneza uimara, usalama na kutukuza taifa lake. Lakini kwa wazi wazi thawabu kubwa zaidi ni kutoka kwa Mwenyezi Mungu Mweza wa yote kwa kutekeleza wajibu wake kwa dini.

Mpendwa Bibi! Kama unapenda uimara na amani kuwepo kwenye familia yako, na mumeo aendelee kukuamini wewe siku zote, kama unajihusisha na haki za wanawake katika jamii; kama unavutiwa na afya ya vijana kiakili na unao wasi wasi kwamba wanaweza wakaacha maadili mema, kama unataka kuchukua hatua za uhakika za wanaume waovu kuacha kuwatongoza wanawake; na kama unatafuta radhi ya Mwenyezi Mungu kwa kuwa Muislamu muaminifu na mwenye kujitolea, basi tumia vazi la Hijabu ya Kiislamu.

Usioneshe uzuri wako na urembo wako kwa wageni, ama uwe ndani nyumbani kwako ukiwa na ndugu zako wa karibu, au kwenye mikusanyiko mingine ya kijamii nje ya nyumbani kwako. Lazima uvae ushungi mbele ya shemeji zako na watoto wao, waume wa wifi zako, waume wa shangazi zako, na binamu zako.

Usipovaa Hijabu ya Kiislamu mbele ya watu waliotajwa ni dhambi na pia unaweza kusababisha mateso makubwa kwa mumeo, hata kama hatasema.

Mwanamke halazimiki kuvaa Hijabu kwa kiwango kile kile mbele ya baba mkwe, kaka yake, na watoto wa kiume wa kaka au dada yake, ingawa ni vema kwa kiwango fulani kuvaa Hijabu mbele ya watu hawa pia. Kwa usemi mwingine, wanawake wasionekane mbele ya watu hawa- ndugu zake- kama ambavyo anaweza kuvaa kwa kumvutia mumewe. Hii ni kwa sababu wanaume wengi sana hawapendi wake zao waonekane katika hali ya kuvutia kwa kuvaa nguo au urembo mbele ya wanaume wengine, na kama mambo yalivyo isisahaulike kwamba utulivu wa akili na imani ya mume kwa mke wake ni muhimu sana kwa kudumu na usalama wa familia yote.