پایگاه اطلاع رسانی آیت الله ابراهیم امینی قدس سره

Kuishi Na Mume

Kazi ya mke ni kumtunza na kumlea mume. Si kazi rahisi. Wanawake hao ambao hawatambui sifa hii ya wajibu wao, wataona vigumu katika kutimiza kazi hii.

Ni kazi ya mwanamke ambaye anatambua kwamba kazi hii inahitaji kiwango fulani cha busara, mtindo na ustadi. Kwa mwanamke kuwa mke aliyefuzu, lazima auteke moyo wa mume wake na kuwa chanzo cha furaha kwake.

Lazima amtie moyo katika kutenda matendo mema na kumshawishi asifanye matendo maovu. Lazima pia mke achukue hatua za kutosha kutunza afya yake na ustawi wake. Matokeo ya bidii yake yanaelekezwa katika kumfanya mume awe mwema na anaye heshimika ambaye atastahili kuwa mlezi wa familia yake, na baba mzuri ambapo watoto watapata mwongozo na heshima. Mwenyezi Mungu, Mjuzi wa yote amemjaalia mwanamke uwezo usio wa kawaida. Mafanikio na furaha, na pia mateso ya familia yapo mikononi mwake.

Mwanamke anaweza kuifanya nyumba kuwa pepo ya hali ya juu au jahanamu inayowaka moto. Anaweza akamfikisha mume wake kwenye kilele cha mafanikio au balaa isiyofaa. Mwanamke mwenye sifa alizopewa na Mwenyezi Mungu, ambaye anatambua wajibu wake kama mke, anaweza kumnyanyua mume wake kuwa mtu wa kuheshimika hata kama alikuwa mtu wa chini sana kuliko wote.

Mwanachuoni mmoja aliandika: Wanawake wanao uwezo wa ajabu ambao kutokana nao wanaweza kupata chochote wanachotaka.”

Katika Uislamu, mke kumtunza mume kuna daraja la maana sana. Imelinganishwa na jukumu la Jihadi (vita takatifu katika njia ya Mwenyezi Mungu). Imam Ali (a.s) alisema: “Jihadi ya mwanamke ni kumtunza mume wake vizuri.”

Fikiria kwamba Jihadi ni mapambano na vita vitakatifu katika njia ya Mwenyezi Mungu, pamoja na mapambano ya kuendeleza heshima ya Uislamu, kulinda nchi za kiislamu na kutekeleza haki katika jamii, ni mojawapo ya matendo ya kiwango cha juu sana ya ibada.

Faida ya kutekeleza majukumu ya mke mzuri, vile vile huakisiwa wakati wa kufikiriwa kwa Jihadi.

Mtume (s.a.w.w) wa Uislamu alisema: “Mwanamke yeyote anayekufa ambapo mume wake yuko radhi naye, huingia Peponi.”

Mtume pia alisema “Kama mwanamke hatatimiza wajibu wake kama mke, hajafanya wajibu wake kwa Mwenyezi Mungu.”