پایگاه اطلاع رسانی آیت الله ابراهیم امینی قدس سره

Msaidie Mume Wako Kupata Maendeleo

Msaidie Mume Wako Kupata Maendeleo

Wanadamu kiasili wanazo nguvu zisizo dhihirika za kuwawezesha kupata maendeleo. Kupenda kupata ubora ni hali ambayo kila mmoja wetu anayo; na tumeumbwa ili tuweze kufanikisha ubora.

Kila mmoja, ambaye anayo kazi yoyote katika umri wowote na katika hali yoyote anaweza kuendelea na kukomaa. Mtu hatakiwi kutosheka na hali ya yeye kuwepo tu na asisahau makusudio ya kuumbwa. Mtu lazima ajaribu kupata ubora katika kipindi cha uhai wake.

Licha ya kwamba kila mtu anafuatilia maendeleo, si wote wanaofanikiwa kupata maendeleo yanayohitaji malengo ya juu na juhudi kubwa ya kufanya kazi. Mtu lazima atayarishe uwanja na kuondosha vigingi na baada ya hapo anachukua hatua muhimu za kuelekea kwenye mkondo wa maendeleo. Umashuhuri wa mwanaume unategemea sana utashi wa mke wake. Mwanamke anaweza kumsaidia mume wake kupata maendeleo kama vile ambavyo pia anaweza kuwa mwenye kusababisha hasara kuhusu maendeleo ya mume wake.

Mpendwa Bibi! Wakati ambapo unafikiria uwezekano, fikiria hadhi ya juu zaidi ya mume wako na umtie moyo wa kufanikiwa. Kama bado anataka kuendelea na masomo yake au kama anataka kuongeza ujuzi wake kwa njia ya kusoma na utafiti, basi usimsitishe. Mpe moyo wa kufanikisha matakwa yake Panga maisha yako kwa namna ambayo hayatakuwa kipingamizi cha maendeleo yake.

Jaribu kumsaidia ili apate maendeleo kwa kutengeneza mazingira ya kuburudisha na kuliwaza ndani ya nyumba yenu. Kama mumeo hakusoma, mshawishi kwa unyenyekevu, mwambie aanze masomo yake ya usiku.

Kama mumeo ni msomi, mtie moyo wa kuongeza ujuzi wake kwa kusoma zaidi.Kama mume wako ni daktari wa tiba, mhamasishe asome majarida ya tiba na makala zingine zinazohusiana na tiba.

Kama mumeo ni mwalimu, mhandisi au jaji, basi mwambie awe anasoma vitabu na makala mbali mbali zinazohusiana na utaalamu wake. Unatakiwa kukumbuka kwamba katika kazi yoyote ambayo anafanya mumeo, ipo fursa ya kuendelea.

Usimruhusu mume wako aache mkondo ambao umewekwa na mpangilio kwenye muumbo. Mtumainishe asome vitabu. Usiruhusu umashuhuri wake usiendelee kuongezeka.

Kama hana muda wa kununua au kupata vitabu basi kwa kutumia ufawidhi wake wa rafiki yake, pata vitabu anavyo vipenda yeye. Mpe vitabu hivyo na mpe matumaini ya kusoma. Wewe pia unatakiwa kusoma vitabu na majarida yenye manufaa. Kama katika kusoma kwako unasoma makala ambayo ina manufaa kwa mume wako, basi mtaarifu. Kitendo hiki kina manufaa kadhaa:

Kwa kufanya hivi mara kwa mara, mume wako atakuwa mtu mwenye kuelimika ambaye atakujengea heshima wewe na yeye. Aidha, atakuwa bingwa mzuri sana ambaye huduma zake zita mnufaisha yeye na jamii yake.

Kwa kuwa amekubaliana na sheria za muumbo, kupitia kwenye masomo na utafiti wake, hapatakuwepo na uwezekano yeye kupata maradhi ya akili na kuchanganyikiwa.

kwa kuwa yupo kwenye mkondo wa kuelekea kwenye maendeleo na anaonesha kupendelea kusoma, basi ataambatana zaidi na wewe na watoto, hatavutiwa kwenye uovu na hatanasa kwenye mtego wa mazoea ya hatari.