پایگاه اطلاع رسانی آیت الله ابراهیم امینی قدس سره

Tabia Za Kupendeza

Mtu yeyote mwenye tabia njema na inayopendeza pia angepata dhiki na matatizo ya maisha kwa njia ile ile. Hawa ni aina ya watu ambao watu huvutiwa nao na wanawatafuta wakati wote. Tabia inayopendeza na msimamo wa mtu utakuwa na kinga dhidi ya maradhi ya kisaikolojia kwa kuwa kuonekana kwao katika maisha ni kushinda matatizo yao kwa njia nzuri iwezekanayo.

Imam Sadiq (a.s) alisema: “Hakuna maisha yanayo kubalika zaidi kuliko yale ambayo yanatokana na tabia njema.”

Lakini mtu mwenye tabia mbaya naye pia angeyaona maisha hayafurahishi kwani uhusiano wa watu hao kuendeleza wasiwasi na fadhaa.

Mtu kama huyu hupenda kulalamika na kupigia kelele maisha. Msimamo wa namna hii huepukwa na watu wengi ambapo mtu huyo hapati marafiki wengi. Hii ndio hali ambayo huathirika kwa urahisi na matatizo mbali mbali ya kisaikolojia na maradhi mengineyo kwa sababu ya wasi wasi na utupu ambao mtu mwenye msimamo mbaya anavyoyaona maisha.

Mtukufu Mtume (s.a.s) alisema: “Mtu mwenye tabia na msimamo mbaya atakuwa kwenye masumbuko na mateso wakati wote.”

Msimamo mzuri na unaopendeza ni muhimu kwa watu wote kwa ujumla na hususan baina ya wanandoa kwani wanandoa lazima wawe pamoja.

Mpendwa Bibi! Kama unataka kufurahia maisha ya furaha na mumeo na watoto wako, ufanye msimamo wako na tabia ya kupendeza vikubalike. Uwe na tabia njema na si mgomvi. Unao uwezo wa kuifanya nyumba yako kuwa Pepo ya hali ya juu au Jahanamu iwakayo moto. Unaweza kuwa malaika wa huruma ambapo mumeo na watoto wanaweza kupata amani kupitia kwako.

Unajua utaacha mvuto wa kupendeza kiasi kwenye roho zao kwa huo msimamo wako wa kutabasamu na lugha nzuri.

Mvuto wa kupendeza ni mbichi katika akili zao wanapoondoka kwenda shuleni au kwenye shughuli za kazi na unawasaidia wao kuwa na mwanzo mzuri wa siku.

Kwa hiyo, kama unajali kuhusu sifa nzuri ya maisha yako na uhusiano ulio nao na mumeo, usiwe kinyume na tabia njema. Uwe dhahiri katika msimamo wako na tabia inayopendeza kwani nguzo bora zaidi ya kutegemea kwa usalama wa ndoa ni maadili mazuri ambayo yanaelekeza kwenye tabia inayopendeza.

Namna nyingi za talaka ni kwa sababu ya tabia zisizolingana za mume na mke. Takwimu juu ya talaka kwa uthibitisho zinaonesha kwamba msimamo wa kupatana, maadili mema na tabia ya kupendeza, hazikuwepo kwa wanandoa husika. Chanzo kikubwa cha ugomvi na kutokuelewana kwa wanandoa ni kwa sababu yakutolingana kwa tabia na kanuni za maadili za wanandoa. Takwimu zifuatazo zinavutia:

“Mwaka 1968 kesi za malalamiko ya ndoa zilizowasilishwa mahakamani zilikuwa 16,039, kesi 12,760 miongoni mwa hizo, misingi ya malalamiko yao ilikuwa kutokulingana kwa kanuni za maadili. Mwaka 1969 kesi za malalamiko ya aina hiyo hiyo 16,058 liziwasilishwa mahakamani, kesi 11,246 miongoni mwa kesi hizo, misingi ya malalamiko ilifanana na ile ya kesi za mwaka wa nyuma. Kwa hiyo, inathibitika kwamba zaidi ya asilimia sabini ya ugomvi wa kifamilia ulisababishwa na kipengele hiki.”

Mwanamke alilalamika kwenye Baraza kwamba mume wake kila siku alikuwa na desturi ya kula chakula chake cha mchana na jioni nje.

Halafu mwanaume akaeleza kwamba sababu iliyomfanya ale nje ni kwamba mke wake hakuwa mbunifu hata kidogo na alikuwa mwenye tabia isiyopendeza kuliko wanawake wote wenye tabia kama hiyo hapa duniani. Haraka sana mwanamke alinyanyuka na kuanza kumpiga mume wake mbele ya majaji.”

Mwanamke huyu mpumbavu alidhani kwamba angebadilisha tabia ya mume wake ya kula chakula chake nje badala ya nyumbani kwa kulalamika, kutukana na kumpiga.

Lakini mwanamke huyu hakutumia mbinu rahisi na ya kiakili ambapo alitakiwa kuwa na busara zaidi na kuzingatia mwenendo unaostahili.

Mwanamke mwingine alipeleka taarifa mahakamani kwamba mume wake aliacha kusema naye kwa muda wa miezi 15 na kwamba alikuwa anatoa matumizi yake kupitia kwa mama yake (mume). Mume alijibu kwamba alikwisha kinai na msimamo usiopendeza wa mke wake ambao ulimfanya yeye asizungumze naye kwa miezi.”15

Migongano mingi ya kifamilia inaweza kusuluhishwa kwa wema, huruma na tabia inayopendeza. Kama mume wako si mwema, kama anatoka kwenda kula chakula cha jioni peke yake, kama anapenda kutumia lugha ya matusi, anatumia utajiri wake wote vibaya, hupenda kusema suala la kutalikiana na kutengana au sababu kadhaa katika ugomvi wa kifamilia, ipo njia moja tu ya kusuluhisha. Njia hii ni kuwa mwema na tabia njema. Matokeo ya mazoea ya tabia kama hii ni ya kimiujiza.

Imam Sadiq (a.s) alisema: “Mwenyezi Mungu Mweza wa yote atampa mtu mwenye tabia ya kupendeza thawabu zinazolingana na zile za Jihadi. Atamneemesha kwa wingi mtu huyo usiku na mchana.”

Imam Sadiq (a.s) alisema: “Mwanamke yeyote anaye msumbua na kumtesa mumewe yu mbali na neema za Mwenyezi Mungu na mwanamke yeyote anayemheshimu, anaye mtii na hamhuzunishi mumewe, ameneemeka na kufanikiwa.”

Ipo hadith inayosema kwamba Mtukufu Mtume (s.a.w.w) alipewa taarifa ya mwanamke mwema ambaye alifunga saumu kila siku na alikuwa anafanya ibada kila siku usiku akimuabudu Mwenyezi Mungu, lakini alikuwa na tabia isiyo pendeza ya kuwaudhi majirani zake kwa maneno yake makali. Mtukufu Mtume alisema: “Hapana jema kwake huyo na yeye ni mkazi wa Jahanamu.”