پایگاه اطلاع رسانی آیت الله ابراهیم امینی قدس سره

Msaada wa kuwalea watoto

Msaada wa kuwalea watoto

Mtoto ni tunda la ndoa. Wote wawili wanamume na wanawake wametoa mchango katika kupatikana kwa mtoto na lazima wagawane matatizo na starehe zinazohusishwa kuwapo kwake. Kumlea mtoto ni kazi ya wazazi wote na si mama peke yake. Ingawa mara nyingi zaidi ni mama ndio wanaolea watoto wao na kuwalisha kuwaweka katika hali ya usafi na kadhalika, baba wasidharau juhudi hizo. Sio sahihi kwa mwanaume kudhani kwamba kazi ya kutunza watoto ni ya wanawake tu na kwamba wanaume hawana wajibu katika jambo hili. Si haki kwamba baba aondoke na kumwacha mke wake na mtoto ambaye analia na aende kupumzika kwenye chumba kingine.

Mpendwa ndugu! Mtoto wako ni wajibu wako pia. Unadhani ni haki kumwacha mkeo na mtoto anayelia ambapo wewe unapumzika kwenye chumba kingine? Hii ni njia inayofaa kufanya mambo nyumbani mwako? Kama vile unavyofanya bidii nje ya nyumba, mkeo hufanya bidii ndani ya nyumba; na anahitaji usingizi kama vile unavyohitaji usingizi. Yeye pia hafurahii kilio cha mtoto, lakini huvumilia.

Ndugu yangu! Ubinadamu halikadhalika na Uislamu unakutaka wewe umsaidie mkeo katika kumlea mtoto wenu. Ama mnatakiwa msaidiane kwa pamoja au mpeane zamu. Kama mkeo anakosa usingizi kwa usiku wote na analala baada ya sala ya alfajiri, halafu usitegemee kwamba atakutayarishia staftahi kama siku zingine. Kwa kweli unatakiwa wewe mwenyewe utayarishe staftahi yako na ya mkeo ili pindi akiamka akute kila kitu tayari mezani. Mke wako hawajibiki kumlea mtoto wenu wakati wote unapokuwa haupo nyumbani au upo safarini. Kwa ufupi unatakiwa umsaidiea mkeo na mgawane wajibu wa kulea mtoto. Kwa njia hii, maisha ya familia yenu yataimarishwa.

Mwisho wanawake lazima pia wakumbuke kwamba waume zao hufanya bidii kupata riziki ya familia na wasitegemee kwamba wanaweza kuwadai zaidi ya uwezo wao. Wanawake wasitegemee waume zao ambao wamechoka kuanza kuwasaidia kulea watoto mara wanaporudi kutoka kazini.