پایگاه اطلاع رسانی آیت الله ابراهیم امینی قدس سره

Mridhishe Na Mliwaze Mke Wako

Mridhishe Na Mliwaze Mke Wako

Pia mwanamke, kama ilivyo kwa mwanamume, hupata mabadiliko ya hisia kubwa. Huhisi furaha, hasira, huzuni na kadhalika. Huchoka kutokana na kazi za nyumbani na inawezekana akaudhiwa na watoto.

Watu wengine wanaweza kumtibua kwa shutuma zao. Inawezekana akaingia kwenye mashindano na wengine. Kwa ufupi, mwanamke hukabiliana na matatizo mengi ambapo mengine miongoni mwa hayo humuathiri sana hivyo kwamba anaweza kukata tamaa kwa kiwango ambacho kitasababisha atoe majibu yasiyofaa hata kwa mambo madogo.

Hususan mfano huu ni kwa upande wa wanawake, kwa sababu wao ni wepesi sana na hutoa majibu kwa umakini zaidi kwa matukio yasiyo pendeza ikilinganishwa na wanume.

Wanawake ambao hupata matatizo huhitaji kutulizwa. Wanaume lazima wawafariji kwa sababu ni wenzi wao na wao ndio wanaoaminiwa na wake zao.

Mpendwa bwana! Unapomwona mke wako katika huzuni na hasira basi jaribu kuelewa hali yake. Kama ukiingia nyumbani kwako na hakusalimu, wewe mtolee ‘salaam’. Tendo hili halita kudhalilisha wewe. Ongea naye ukiwa katika tabasamu. Epuka ukali. Msaidie kazi za nyumbani. Uwe mwangalifu usimuudhi kwa namna yoyote. Usimtanie. Kama hajisikii kuzungumza, basi mwache. Usiseme: “Unasumbuliwa na nini?”

Kama anayo hali ya kutaka kuzungumza, msikilize na mliwaze. Jifanye unahusika zaidi na tatizo lake kuliko yeye. Mruhusu akwambie malalamiko yake kwako. Halafu, kama vile baba mwema au mume mwenye huruma jaribu kumsaidia apate ufumbuzi wa tatizo lake. Mpe moyo wa kuwa mvumilivu. Kwa busara na mantiki mfanye ayaone matatizo yake kama madogo. Imarisha tabia yake na msaidie kushinda sababu ya hasira yake, uwe mvumilivu na mtendee kufuatana na mantiki yako. Kwa hakika atauona, msaada wako kuwa unafaa na maisha yatarudi katika hali yake ya kawaida baada ya muda mfupi kwenu nyinyi wote.

Kinyume chake, ukimwendea isivyo sahihi, inawezekana ukasababisha mateso zaidi kwake. Pia wewe utateseka na inaweza kusababisha ugomvi mkubwa ambao utawapa usumbufu wote wawili.