پایگاه اطلاع رسانی آیت الله ابراهیم امینی قدس سره

Mlezi wa Familia

Mlezi wa Familia

Mwanaume na mwanamke ni nguzo mbili za msingi wa familia, lakini kwa kuwa wanaume wamepewa sifa maalum kwa amri ya uumbaji, na kwa sababu ya uwezo wao wa mantiki ni imara zaidi ya ule wa wanawake, wao huchukuliwa kama walezi wa familia zao.

Mwenyezi Mungu Mweza wa yote amewaweka wanaume kuwa walezi wa familia zao na anasema kwenye Qur’ani:

    الرِّجَالُ قَوَّامُونَ عَلَى النِّسَاءِ بِمَا فَضَّلَ اللَّهُ بَعْضَهُمْ عَلَىٰ بَعْضٍ

“Wanaume ni wasimamizi wa wanawake, kwa kufadhiliwa na Mwenyezi Mungu baadhi yao juu ya baadhi … (Quran 4:34)”

Kwa hiyo, wanaume wana jukumu kubwa na zito zaidi katika kuzisaidia familia zao.

Ni mwanaume ambaye kwa kutumia busara yake, anaweza kuisadia familia yake na kutayarisha mazingira kwa ajili ya furaha yao, na ni yeye ambaye anayeweza kuigeuza nyumba kuwa Pepo na mke wake kuwa kama Malaika.

Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w.w) alisema: “Mwanaume ni mlinzi wa familia yake na kila mlezi anao wajibu kwa hao waliopo kwenye ulinzi wake.”

Mwanaume ambaye anaisaidia familia yake, lazima atambue kwamba mwanamke pia ni binadamu kama mwanaume. pia mwanamke anayo matamanio na haki ya uhuru na maisha. Kumuoa mwanamke si kukodisha mtumishi, lakini ni chaguo la mwenza na rafiki ambaye atakuwa tayari kuishi pamoja katika maisha yote. Mwanaume lazima amtunze na amtimizie matakwa yake. Mwanaume si mmiliki wa mke wake, kwa kweli mwanamke anazo haki fulani kwa mume wake. Mwenyezi Mungu anasema kwenye Qurani Tukufu:

    وَلَهُنَّ مِثْلُ الَّذِی عَلَیْهِنَّ بِالْمَعْرُوفِ ۚ وَلِلرِّجَالِ عَلَیْهِنَّ دَرَجَةٌ ۗ وَاللَّهُ عَزِیزٌ حَکِیمٌ

“...Nao wanawake wanayo haki kwa sharia kama ile haki iliyo juu yao. Na wanamume wana daraja zaidi kuliko wao…” (Quran 2:228)